Bujumbura, Burundi. Huku Serikali ikikanusha
kuhusika katika mauaji ya kiongozi wa upinzani wa Burundi, baadhi ya
makundi ya kisiasa yameanza kuingiwa na wasiwasi kuhusiana na hatima ya
kisiasa ya nchi hiyo, wiki moja baada ya Rais Pierre Nkurunziza kusogeza
mbele tarehe uchaguzi wa wabunge.
Kiongozi mwandamizi wa upinzani, Agathon Rwasa
alisema kuwa hakuna taarifa rasmi kuhusu ni nani aliyetekeleza mauaji
hayo ingawa alisema kuwa mwanasiasa huyo alikuwa mstari wa mbele kupinga
mkakati wa Rais Nkurunziza kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Post a Comment