Christy Sims
ni mwanadada ambaye maisha yake yalibadilika ghafla baada ya aliekuwa
mpenzi wake wa muda mrefu kumuachia majeraha ambayo hatokuja kuyasahau
maishani.
Akiwa na miaka 40 Christy
amelazimika kuishi na makovu baada ya kumwagiwa tindikali na
ex-boyfriend wake kwa sababu tu ya wivu wa mapenzi, kumhisi kuwa
anatembea na mtu mwengine.
Haya yote yalitokea weekend moja ya mwaka 2013 nyumbani kwa mpenzi wake ambaye aliamua kumwagia dada huyu tindikali usoni, kifuani na mikononi kitendo kilichosukumwa na hasira kali za wivu.
Christy alipiga
kelele nyingi na kuomba msaada lakini boyfriend wake aliamua kumuacha
aungue mpaka watu wa huduma ya kwanza walipofika na kushangazwa kwa nini
boyfriend huyo hakuchukua hatua za kumpatia girllfriend wake huduma ya
kwanza.
Post a Comment