Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

LOWASA NA MEMBE HURU URAIS 2015!!!!!

 LOWASA NA MEMBE HURU URAIS 2015!!!!!

Dodoma. Mpambano mkali wa kuwania nafasi ya kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM sasa umeanza rasmi baada ya Kamati Kuu ya chama hicho tawala kuwaweka huru makada sita waliokuwa wamefungiwa kwa takriban miezi 17 kwa makosa ya kukiuka kanuni za uchaguzi.
Kufunguliwa kwa makada hao, ambao baadhi yao wanapewa nafasi kubwa ya kupitishwa na chama hicho, kumekuja wakati CCM ikikabiliwa na tishio la kutokea mgawanyiko mkubwa, hasa kutokana na baadhi ya kambi kuituhumu sekretarieti kuwa inabagua baadhi ya wagombea.
Makada waliofungiwa tangu Februari, 2014 kwa kosa la kuanza kampeni mapema ni mawaziri wakuu wa zamani, Frederick Sumaye na Edward Lowassa, ambaye kwa sasa ni mbunge wa Monduli.
Wengine ni Bernard Membe, ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Steven Wasira (Waziri wa Kilimo na Chakula), January Makamba (Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia), na mbunge wa Sengerema, William Ngeleja.
Baadhi ya wanachama wa CCM, hasa wajumbe wa Halmashauri Kuu, walianza kumiminika nyumbani kwa makada hao mara baada ya kupata taarifa za kuondolewa kwa adhabu hiyo, wengi wakionekana kwenda kumpongeza Lowassa.
Kufunguliwa kwa makada hao ni mwanzo wa kinyang’anyiro kikali cha kuwania kumrithi Jakaya Mrisho Kikwete kwenye nafasi ya urais na mwenyekiti wa chama hicho kikongwe na dalili zote za kuwapo kwa vita kali zilianza mara moja jana baada ya kutangazwa kwa uamuzi huo.
Image result for lowassaImage result for membe
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Heka Heka Zangu
Back To Top